FAHAMU UGONJWA WA BAWASIRI - MAINTAIN YOUR HEALTH

Trending

Thursday, October 12, 2017

FAHAMU UGONJWA WA BAWASIRI








                                                                                         I.        UTANGULIZI


Bawasiri ni ugonjwa ambao unatokana na kuathirika kwa mishipa ya sehemu ya ndani na nje ya tundu la haja kubwa na wakati mwingine kutoa damu wakati wa kutoa haja kubwa. Ugonjwa huu unasababisha muwasho na maumivu makali katika tundu la haja kubwa. 

Mara nyingi tatizo hili huwapata watu kuanzia umri wa miaka 30 – 70.  


Kuna aina mbili za bawasili:
  1. Bawasiri ya Ndani: Hiki nikinyama kinachootea ndani kabra hakijatokea njee.
  2. Bawasiri ya Nje: Hiki nikinyama au kivimbe kinatokea njee baada yakutokea ndani. Kinatokea njee kwawalio athirika, na ukikaa muda mrefu nahuu ugonjwa unajikogotea matatizo ya kiafya ambayo siyo rahisi kukabiriana nayo, na maranyingi ugonjwa huu unasababisha vifo vya gafla.


                                 II.        CHANZO CHA UGONJWA WA BAWASIRI


Bawasiri ni tatizo linaloanzia kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Huu mfumo ukishakua mbovu unakuperekea kutokupata cho vizuli.

Mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula unasababisha chakula kisimeng'enywe vizuri kwenye utumbo mdogo na hivyo kupelekea chakula kupiliza kwenda moja kwa moja kama kilivyo kwenda kwenye utumbo mkubwa ambapo maji maji kutoka kwenye chakula hufyonzwa na kuacha chakula kikiwa kikavu.Inapofikia wakati wa kupata choo; choo kinakua kikavu hivyo unatumia nguvu nyingi kukisukuma choo kitoke. Sasa kitendo hicho kinapelekea misuli ya haja kubwa kutanuka na kupelekea kukwanguliwa na choo kigumu na hivyo kinyama kuanza kujitengeneza, na hapo ndipo utaanza kusikia maumivu na miwasho kwa ndani, na mara nyingine kupata choo chenye damu.Kadri unavyoendelea kupata choo kigumu misuli inaendelea kukwanguliwa na kinyama kuongezeka mpaka kinatokezea nje na hicho kinyama kinaitwa Bawasiri (Hemorrhoids).Mtu anastahili kupata choo kulingana na milo anayetumie kila siku. Mtu mwenye afya nzuri anapata choo kulingana na milo aliopata kwa siku. Kama unauwezo wakupata milo mitatu kwa siku, unasitahili kupata choo mara tatu kwa siku, tena choo chako kitoke na urefu sawa wa ndizi mbivu, bila kujikatakata kama kile cha mbuzi. 


Hivi ni baadhi ya vitu vingine vinaperekea mtu kupatwa na ugonjwa wa bawasili.

  • Kufanya mapenzi kinyume na maumbile·         
  • Kuharisha kwa mda mrefu·         
  • Tatizo la kutopata choo laini au kujisaidia kinyesi kigumu,·         
  • Kinyesi cha kujikatakata kama kile cha mbuzi·         
  • Tatizo la umri mkubwa·         
  • Uzito kupita kiasi (Uzito uliopindukia)
  • Matumizi ya vyoo vya kukaa au vya kuchangia

 



                 III.        DALILI ZA UGONJWA WA BAWASIRI – CHUKUA TAHADHARI MAPEMA
 


-       Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa. Huu muasho unakuja kwa kujirudia mara kwa mara baada ya muda furani.


-       Kukatishwa kwa haja kubwa na kurudi ndani wakati wa kujisaidia. Hiki kitendo nikibaya sana.


-       Kujitokeza kwa uvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa. Uvimbe huu unaanza kuota kama uperepere.


-       Kujitokezea kwa kijinyama katika tundu la haja kubwa. Kinyama hiki kinaanzia ndani ya tundu la haja kubwa. kikitokea nje, ujue kwamba una hili tatizo la bawasili kwa muda mrefu, na linaweza kusababisha vifo vya gafla kwa sababu mishipa inayosafirisha damu ndio inakwanguliwa na mwishoe kuathirika. Chukua tahadhari mapema kabra hujaathirika sana au upoteze maisha; kwasababu hiki ni chanzo   cha kupatwa na magonjwa mengine mengi ya kiafya.


-       Kujisaidia kinyesi chenye damu na kunuka kwa harufu mbaya sana


-       Kupumua (kujamba) kiasi kwamba mwezako hawezi kuvumilia hali iliotokea ya uchafuzi wa mazingila
 



          IV.        MADHARA YA UGONJWA WA BAWASILI – 
                  CHUKUA  TAHADHARI NA HATUA MAPEMA
 

  • Upungufu wa damu mwilini
  • Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa na kusababisha mishipa ya sehemu ya haja kubwa kukwanguliwa.
  • Kuna uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya utumbo (Cancer) kwasababu kile kinyama kinakaa kama kidonda
  • Kutopata hamu ya tendo la ndoa kwa jinsia zote.
  • Upungufu wa nguvu za kiume kwa mwanamume, ikiwemo uume kushindwa kusimama kwa muda unaotakiwa na kushindwa kurudisha heshima ya ndoa.
  •  Uume kusinya (unapoteza urefu na ukakamavu)
  • Sperms (Mbegu za mwamume) kutokua bora kiasi kwamba haziwezi kumpa mimba mwanamuke, au kusababisha mimba kutoka kila wakati.
  • Kuathirika kisaikolojia
  • Kutojiamini katika hadhara ya watu

  


                    V.        JINSI YA KUDHIBITI TATIZO HILI LA BAWASILI (HEMORHOIDS  ) KABRA HALIJAKUPATA

 






  • Jitahidi kupata mlo kamili kila siku. Tutumia matunda na mboga za majani kwa wingi (kila mlo).
  • Kunywa maji ya kutosha. Angalau lita 3 kwa siku.
  • Epuka kukaa chooni kwa mda mrefu
  • Jiepushe na vilevi
  • Usiwe mpenzi wavitu vya viwandani
  • Jenga utaratibu wa kusafisha mwili wako kwakutumia Cleansing Program, ili utoe taka mwili zote, na uondoe sumu mwilini; kama vile unavyooga zaidi ya mara mbili kwa siku. (Wasiliana na si kwauhitaji wa program ya kusafisha mwili, kuondoa sumu na kupunguza mafuta mwilini)
 


                                                VI.        NJIA ZAKUONDOA TATIZO HILI
 


a.    Tiba yake hospitalini Ugonjwa huu tiba yake ni opereation (kukukata uvimbe uliojitokeza katika tundu la haja kubwa ili usiendelee kukua na kusababisha magonjwa mengine. Lakini tiba hii si nzuri kwani hupelekea kujirudia tena kwa uvimbe pale mgonjwa akosapo kinga tosha mwilini. Pia hupelekea maumivu makali kwa mgonjwa, na baadae tatizo hili kujirudia kwa kasi kubwa. Operation ya Bawasili ni bei gali mnoo, sio wote wanaopata furusa hii hata kama sio nzuri kiafya. b.    Tiba nzuri ni kutumia lishe na virutubisho (mwili utajitengenezea kinga bora tena yakudumu)


Tiba nzuri ni kuanda utaratibu wa kusafisha mfumo wako mzima wa mumeng’enyo wa chakula (Digestive System) kwa njia asilia bila kutumia makemikali yeyote.
Chanzo cha magonjwa yote tunayoyapata anatokana na mfumo mbovu wa mumeng’enyo wa chakula na mzunguko wa damu (Poor Blood Circulation).Kila siku tunaoga zaidi ya mara mbili kwa siku, pia nakuosha magari yetu ,… n.k. vivyo hivyo tunapaswa kuanda utaratibu wakusafisha mili yetu na kuhakikisha sehemu kuu tatu za mili yetu zinafanya kazi vizuri sana. 




VII.        Umuhimu wa kuboresha na kuimarisha sehemu kuu mbili za                                                                 mwili

 

1.    Digestive System (Mfumo mzima wa mumeng’enyo wa chakula) 


 

2.    Blood Circulation (Mfumo mzima wa mzunguko wa damu)
 

 


Kwa wale wote ambao wanahitaji kusafisha mfumo mzima wa mumeng’enyo wa chakula, kuweka sawa mfumo mzima wa mzunguko wa damu, na kuondoa au kudhibiti tatizo la bawasiliili waondokane na miwasho, maumivu na vimbe zilizojitokezea katika sehemu hiyo ya haja kubwa“Wasiliana nasi kwa namba zifuatazo hapo chini.”

 N.B: Kabra hujawasiliana nasi jua kwamba, bidha zetu sio dawa bali ni Virutubisho vyenye Carbohydrates & Proteins, Vitamins & Mineral, Essential Fatty Acids, Trace Elements. Hivi ndo vitu mwili wetu unahitaji kuvipata ili uzidi kutengenza kinga ya mwili kwajili ya kujiepusha na magonjwa mbali mbali, na hivi vyote tungepaswa kuvipata kupitia vyakula tunavyo kula kila siku. Lakini kulingaa na mfumo wa maisha jinsi ulivyo, hatupati vitu muhimu mwili unahitaji.  Ukitumia bidha hizi hutahangaika na kutafuta vitu mbali mbali ili utengeneze mlo kamili, pia mwili utatengeneza kinga na baadae afya yako itaboreka na kuimarishwa. Vitu vyote mwili unahitaji vimeandaliwa kiasilia bila kemikali yeyote.

BAWASIRI NI UGONJWA HATARI KAMA HUTOUCHUKULIA HATUA YA TIBA MAPEMA.


Kwa maelezo zaidi au uhitaji wa program hii. Wasiliana nasi kwa namba zifuatazo:


     +255 657 261124, +255 738 651373








2 comments:

  1. Somo muhimu sana wengi hawana Elim hii, wengine tunaishia kumeza dawa za kuharisha kumbe tunaongeza tatizo. Asante sana

    ReplyDelete

Post Top Ad

Responsive Ads Here